MYDUKA ONLINE
WhatsApp

Blog ya biashara

Kwa Nini Unahitaji Blog ya Biashara.

Teknolojia imeleta mapinduzi makubwa kwenye biashara, na moja ya nyenzo muhimu za kufanikisha biashara mtandaoni ni kuwa na blog ya biashara. Hii siyo tu sehemu ya kushare taarifa, bali ni silaha madhubuti ya kujenga uaminifu, kuongeza SEO na kufikia wateja wapya kila siku.

1. Kuongeza Uonekano Mtandaoni (SEO)

Blog hukuwezesha kuandika makala zenye keywords muhimu zinazotafutwa na watu Google. Kadri unavyoandika zaidi, ndivyo tovuti yako inavyoonekana zaidi kwenye matokeo ya utafutaji.Hali inayopelekea blog yako kuonekana na watu wengi hivyo kuongeza trafiki kwenye blog yako na kufuatiliwa na watu wengi.

Mfano: Ukitengeneza post yenye kichwa “Jinsi ya kuuza bidhaa za mtumba mtandaoni Tanzania”, watu wanaotafuta hilo wanaweza kuipata blog yako kwa urahisi na kuona maudhui yanayoendana na utafutaji wao.

2. Kujenga Uaminifu kwa Wateja

Wateja hupenda kufanya biashara na mtu anayejua anachofanya. Blog huonyesha utaalamu wako kwa kuandika makala zinazosaidia wateja.Hali inayojenga uaminifu na kuwafanya watu wavutiwe na kufuatilia maudhui mbalimbali kutoka kwenye blog yako .

Mfano: Ukiandika post kama “Faida za kutumia WhatsApp Business”, unamshawishi mteja kuwa wewe ni mtaalamu wa biashara ya kisasa kwa kuweza kutumia vyema app ya whatsap business katika kukuza biashara yake.

3. Kuelimisha na Kutoa Thamani

Badala ya kuuza tu bidhaa, blog hukuwezesha kutoa elimu kwa wateja wako kuhusu jinsi ya kutumia bidhaa zako au kutatua changamoto zao.kwahiyo inasaidia kuongeza maarifa Kwa wateja wako kuhususiana na mada husika hivyo unawafanya waweze kujifunza na kufahamu mambo ambayo walikuwa hawafahamu awali.Hali inayopelekea kuwaongezea maarifa juu ya jambo fulani ambalo walikuwa hawalijui.

4. Kuongeza Trafiki kwenye Tovuti

Kila makala mpya ni kama mlango mpya kwa wageni kuingia kwenye tovuti yako. Blog yenye makala nyingi huleta trafiki ya bure kila siku.Kwahiyo makala mapya marakwamara humshawishi mteja kuvutiwa na kutembelea blog Yako mara Kwa mara Ili kupata taarifa mpya zinazohusiana na blog yako.Hali inayopelekea kuongeza trafiki katika blog yako.

5. Kusaidia Mauzo Kupitia Maudhui

Unaweza kutumia blog kuelezea faida za bidhaa zako na kutoa link za kununua moja kwa moja. Hii huitwa content marketing.Ambapo unafanya mauzo kulingana na maelezo ya bidhaa husika.Mara Nyingi ni ngumu mteja kununua bidhaa ambayo Haina maelezo yanayoifafanua bidhaa husika.Lakini bidhaa ikiwa na content ni rahisi kumshawishi mteja kufanya manunuzi hasa baada ya kusoma maelezo ya bidhaa husika na kuyaelewa.Hali inayopelekea ushawishi mkubwa kwa mteja kuweza kununua kulingana na sifa sahihi za bidhaa husika.

6. Kujenga Jamii ya Wafuasi

Watu wanaopenda maudhui yako wataendelea kurudi na hata kushirikisha wengine. Blog inaweza kukusaidia kuanzisha community ya wafuatiliaji wa biashara yako.Amapo itakusaidia kuongeza mauzo na kujenga Imani Kwa wateja wako.Katika dunia ya leo, maudhui ndiyo mfalme. Biashara zinazotoa maudhui bora ndizo zinazoshinda sokoni. Blog ni jukwaa lako binafsi la maudhui ya biashara Yako mtandaoni.

Hitimisho

Kama unataka biashara yako ivume mwaka huu, usikose kuwa na blog ya biashara. Kuwa na blog yako ni njia bora ya kukuza jina la biashara yako, kuvutia wateja, na kuongeza mauzo bila kutumia gharama kubwa ya matangazo.

Unasubiri nini? Anza blog yako leo!

Ikiwa una ndoto/ mpango/ malengo ya kumiliki blog Yako karibu tupo Kwa ajili yako.

EADRYC Boxer

©E-ONLINE

Jiunge nasi Katika group letu la Whatsapp ili kupata update za makala mbalimbali kila yanapotoka.Karibu sana!!!

Jiunge sasa